Aya
9
Mahali iliteremshwa
Makka
SURAT AL-HUMAZAH
(Imeteremka Makka)
Katika Sura hii kipo kitisho kikubwa kwa mwenye kuzoea kuwakebehi watu kwa ishara au kwa maneno, mwenye kukusanya mali mengi, akayahisabu kwa ajili ya fakhari, na kudhani kuwa mali yake yatambakisha milele duniani.
Na humo vile vile lipo onyo kubwa kwa hao kuwa watatiwa kwenye Moto mkali unao vuruga miili yao na nyoyo zao, na wanafungiwa milango, na juu ya hivyo watafungwa pingu humo basi hawataweza kutaharaki wala kutoka.