Aya
6
Mahali iliteremshwa
Makka
SURAT AL-KAFIRUN
(Imeteremka Makka)
Katika Sura hii Mwenyezi Mungu anamuamrisha Mtume wake s.a.w. awakatishe tamaa makafiri katika juhudi zao za kutaka kusikilizana na Mtume katika wito wake wa Haki, kwa kuwa yeye ni mwenye kubakia vile vile juu ya ibada ya Mwenyezi Mungu ambaye hapana mungu ila Yeye, na wao wabakie kuiabudu miungu yao ambayo haifidi chochote katika Haki, wao wawe na dini yao walio ifuata baba zao, na yeye na Dini yake aliyo mridhia Mwenyezi Mungu aifuate.